Thursday 6 March 2014

BEKI wa kati wa Yanga, Kelvin Yondani ‘Vidic’, ameibuka na kudai kuiua Al Ahly kwao inawezekana kabisa, lakini itakuwa hivyo kama tu wachezaji wote watacheza kwa ushirikiano na kusaidiana uwanjani pindi mambo yanapokuwa magumu.

“Tumefanya mazoezi vizuri na tupo tayari kwa mapambano, sisi ni kama wanajeshi, tunakwenda vitani hatuhofii chochote, tutahakikisha tunapambana vilivyo kuhakikisha tunashinda mechi hiyo na kukomesha utawala wa wapinzani wetu,” alisisitiza.
“Sioni kitu cha kuhofia kwani hapa nyumbani wengi hawakutupa nafasi ya kushinda, lakini tukashinda (bao 1-0) hivyo hata ugenini tunaweza kushinda hasa kama kila mchezaji atatambua majukumu yake uwanjani.
“Tunapaswa tukacheza kwa umoja na ushirikiano na yeyote atakapoona mwenzake mambo yamemzidi, basi mara moja achukue jukumu la kumsaidia ili kuhakikisha malengo yetu yanatimia.”

No comments:

Post a Comment