Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza kikosi cha wachezaji 22
kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya kalenda ya FIFA dhidi ya Namibia
(Brave Warriors) itakayochezwa Machi 5 mwaka huu jijini Windhoek,
Namibia.
Wachezaji
walioitwa katika timu hiyo ni makipa Deogratius Munishi (Yanga), Ivo
Mapunda (Simba) na Mwadini Ally (Azam). Mabeki wa pembeni ni Edward
Charles (JKT Ruvu), Erasto Nyoni (Azam), Hassan Mwasapili (Mbeya City)
na Michael Aidan (Ruvu Shooting).
Mabeki
wa kati ni Aggrey Morris (Azam) na Kelvin Yondani (Yanga) wakati viungo
ni Amri Kiemba (Simba), Athuman Idd (Yanga), David Luhende (Yanga),
Frank Domayo (Yanga), Jonas Mkude (Simba) na Mwinyi Kazimoto (Markhiya
Sports Club, Qatar).
Washambuliaji
ni Athanas Mdamu (Alliance Mwanza), Haruna Chanongo (Simba), Khamis
Mcha (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-
DRC), Mrisho Ngasa (Yanga), Ramadhan Singano (Simba) na Thomas
Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC).
No comments:
Post a Comment