WAKATI Chama Cha Mapinduzi (CCM), kikiweka msimamo wa kupinga muundo
wa serikali tatu, baadhi ya wajumbe wameelezwa kusikitishwa na mjadala
kujikita kwenye muundo wa serikali.
Wakizungumza na Tanzania Daima jana, walisema mazungumzo
makubwa yaliyotawala ni muundo wa serikali badala ya kufikiria kujadili
mambo muhimu yenye masilahi ya taifa.
Mmoja wa wajumbe hao, Dk. Pudenciana Kikwembe alisema ni vema kwa
sasa wajumbe wakawaza mambo yenye masilahi kwa taifa badala ya
kufikiria zaidi ya masuala ya Muungano.
“Hapa napata mashaka sana kama kweli katiba hii itakuwa na maana
kwa Watanzania walio wengi kama kweli tutaendelea na msimamo ambao
unaonekana kujengeka kwa wajumbe wengi ambao wapo katika bunge hili.
“Kila mtu akili yake inawaza zaidi juu ya muundo wa serikali, lakini
sijasikia kama kuna watu ambao wanajikita zaidi katika masuala ya
msingi na kuonyesha nia ya wajumbe kuweka vipaumbele ambavyo
vitawafanya Watanzania kunufaika kutokana na rasilimali zao.
Job Ndugai, alisema Bunge hilo hivi sasa linaonekana litatawaliwa na
mijadala mikali kuhusu muundo huo na mamlaka ya rais kwa kuwa mambo
hayo yamepewa msukumo mkubwa na wanasiasa na vyombo vya habari.
Alisema tayari mambo yameshaanza kuonekana yatakuwa magumu katika
hatua za awali ambapo wabunge wengi walikuwa wakijadili bila utaratibu
huku wengine wakionekana kubeba misimamo yao.
“Si vibaya kuwa na msimamo lakini cha msingi hapa tunatunga Katiba
ya taifa, hivyo ni lazima tubishane kwa hoja na kushawishiana kwa lengo
la kutengeneza Katiba Mpya nzuri zaidi,” alisema.
No comments:
Post a Comment