KIONGOZI wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe amesema
kuwa ushiriki wake katika kamati iliyoundwa kuweka msimamo kuhusu posho
za wabunge umesaidia sana kuhakikisha msimamo wa chama chake
unawasilishwa na kuamua hatima ya suala hilo ambalo limeteka mjadala wa
kisiasa nchini.
Mbowe, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA), alisema hivyo akijibu baadhi ya hoja zilizokuwa zikitolewa na
wanasiasa na wananchi kadhaa kwamba asingekubali kuingia katika kamati
hiyo.
Waliopinga ushiriki wa Mbowe kwenye kamati hiyo walitaka ajiondoea
kwani CHADEMA kilishaweka msimamo kuwa hakuna haja ya kuongeza posho.
No comments:
Post a Comment